Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, September 30, 2013

KENYA YAINGIA VITANI...!!!


 
  Serikali ya Kenya, imesema nchi hiyo ipo katika vita na wapiganaji wa jihadi kutoka nchini Somalia Al Shabaab.Pia Serikali nchini humo imekanusha taarifa zinazodai k uwe p o kwa s h amb u l i o linalodaiwa kufanywa na Al Shabaab katika jengo la kibiashara la Westgate, Septemba 21 mwaka huu, zilipuuzwa

. Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), watu 67 walipoteza maisha katika shambulio hilo ambalo lilidumu kwa siku nne ndani ya jengo hilo.Juzi usiku, Wakenya na raia wa nchi nyingine waliopoteza ndugu zao katika shambulio hilo, waliwasha mishumaa nje ya jengo hilo ili kuwakumbuka waliokufa.   Magazeti ya Kenya yalidai Idara ya Usalama nchini humo ilitoa ilani mwaka mmoja uliopita juu ya watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa Al Shabaab, kupanga kufanya mashambulizi Mjini Nairobi na Mombasa. 

Sunday, September 29, 2013

MAJAMBAZI WAVAMIA BENK JIJINI DAR ES SALAAM NA KUPORA ZAIDI YA MILIONI 150..


Majambazi saba akiwemo mmoja ambaye amevalia sare za polisi wameiteka benki ya I&M  jijini Dar es Salaam na kuchukuwa fedha zinazohisiwa  kuwa  ni zaidi ya shilingi milioni 150 na kutokemea kusikojulikana.

Tukio hilo limetokea katika benki hiyo iliyoopo katika makutano ya mtaa wa Indira Gandi na Mosque ambapo baadhi ya mashuhuda wameelezea tukio hilo lilivyokuwa.

Saturday, September 28, 2013

Tume ya Warioba yatishia kujiuzulu....!!!

Mzee Joseph Butiku na Profesa  Mwesiga Baregu
TUME ya Mabadiliko ya Katiba inayoongozwa na Waziri Mkuu wa zamani, Jaji Joseph Warioba, sasa inasuburi uamuzi wa mwisho wa serikali kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba uliopitishwa hivi karibuni bungeni, ili hatimaye kwa pamoja wajumbe wa tume hiyo waamue kujiuzulu ama waendelee na majukumu yao, Raia Mwema limeelezwa.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu mbalimbali vya habari ndani ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, katika kikao chake cha mwanzoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam, sehemu kubwa ya wajumbe walikuja juu wakionyesha kukerwa na namna mabaraza ya katiba yalivyoingiliwa na Chama cha Mapinduzi.

Mali ya bilioni tisa yauzwa kwa milioni 243/-

Makao Makuu Consolidated Holding Corporation (CHC)
UTATA umegubika uuzwaji wa iliyokuwa bohari ya serikali ya Chang’ombe, Dar es Salaam inayokadiriwa kuwa na thamani ya Sh bilioni tisa lakini ikiwa imeuzwa kwa thamani ya Sh milioni 243 tu, Raia Mwema, limebaini.
Hata hivyo, wakati nyaraka za gazeti hili zikionyesha mauzo ya Sh. milioni 243, mrithi wa PSRC iliyokuwa ikisimamia mali hizo na nyingine za serikali chini ya mchakato wa ubinafsishaji, Consolidated Holding Corporation (CHC) taarifa zake rasmi zinaeleza bohari hiyo imeuzwa kwa Sh. milioni 195.9.

KUFUNGIWA KWA MAGAZETI YA MWANANCHI NA MTANZANIA KWA MUDA ......

...






Serikali imeyafungia kutochapishwa Magazeti ya MWANANCHI na MTANZANIA kuanzia 27 Septemba, 2013 kutokana na mwenendo wa magazeti hayo kuandika habari na makala za uchochezi na uhasama kwa nia ya kusababisha wananchi wakose imani kwa vyombo vya dola hivyo kuhatarisha amani na mshikamano ulipo nchini.

Gazeti la MWANANCHI limefungiwa kutochapishwa kwa siku kumi na nne(14) kuanzia 27 Septemba,2013.Adhabu hii imetangazwa kwa Tangazo la Serikali(Government Notice )Namba 333 la tarehe 27 septemba,2013.

Friday, September 27, 2013

MUHIMU:Jifunze mpangilio wa Chakula kwa wanamazoezi..!!

 Mazoezi yana umuhimu mkubwa kwa maisha yako endapo utaweza kuyafanya kwa jinsi ipasavyo
Kujua muda wa kula na kitu cha kula kunaweza kukusaidia kupata matokeo tofauti katika ufanyaji wako wa mazoezi.
Wanasayansi wanasema kuwa ulaji na mazoezi ni vitu vinavyoenda bega kwa bega. Ni vizuri kuelewa chakula unachokula kinaathiri vipi mazoezi yako.

Warioba: Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ina upungufu..!!!


Dar es Salaam. Wakati wananchi wa kada mbalimbali wakishinikiza Rais Jakaya Kikwete kutokusaini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba 2013, kwa maelezo kuwa una kasoro, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba naye amesema sheria ina upungufu.
Warioba alisema jana kwamba ni jambo la kushangaza sheria hiyo kueleza kuwa tume hiyo itavunjwa baada ya kukabidhi Rasimu ya Katiba kwenye Bunge Maalumu la Katiba, wakati huohuo ikieleza kuwa itahusika tena kusimamia utoaji wa elimu ya kura ya maoni.

Wednesday, September 25, 2013

Mwanamke aliyeongoza shambulizi la kigaidi la Westgate adaiwa kuuawa


Dar es Salaam/Nairobi. Huku mapambano yakiwa yamepamba moto, anayedaiwa kuwa Kiongozi wa kundi la magaidi lililovamia jengo la kibiashara la Westgate, Samantha Lewthwaite inadhaniwa kuwa ameuawa.
Lewthwaite, ambaye anaitwa kwa jina la utani la ‘Mjane Mweupe’ anadaiwa kuongoza shambulizi hilo lililosababisha vifo vya watu 62 na kujeruhi wengine 170 mjini Nairobi.

Wanawake wawili wakamatwa na maiti yenye madawa tumboni!!!


Wanawake wawili Nasra Omari (36) na Mwanaisha Kapama (36), ambao ni wakazi wa Kigogo Luhanga, jijini Dar es Salaam wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kukutwa na maiti iliyokuwa na dawa za kulevya (aina ya heroin pipi 33 zenye thamani ya mamilioni ya fedha) tumboni.

Marehemu alikutwa na hati ya dharura ya kusafiria nchi za nje ambayo haikuonyesha anakoelekea.Wanawake wawili wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kukutwa na maiti iliyokuwa na dawa za kulevya tumboni.

Friday, September 20, 2013

HATARI:DAWA ZA KULEVYA SASA KUCHANGANYWA NA SUMU YA PANYA


Dawa mpya ya Kulevya inaitengesha jamii nchini humo.
Nyaope ni dawa ya kulevya yenye mchanganyiko wa vitu vingi, na bei yake haifikii hata Dola Mbili na Nusu, lakini inaathiri maisha ya vijana wengi.
Uhalifu unaohusihwa na dawa za Kulevya unaongezeka Afrika Kuisni. Watu wameitaka serikali kushughulikia vyema suala hili. Suluma Kassim anasimulia
TAZAMA VIDEO HAPA

Wednesday, September 18, 2013

WALIOLIPUA MABOMU KWENYE MKUTANO WA CHADEMA JIJINI ARUSHA WAKAMATWA...!!


 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw Magesa Mulongo. 

WATUHUMIWA walioingiza mabomu ya kurushwa kwa mkono yaliyotupwa Arusha Mei na Juni katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti na kwenyemkutano wa wa hadhara wa Chadema, Soweto mkoani Arusha, wamekamatwa.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, alisema hayo jana katika mkutano wa siku moja wa kuzungumzia fursa za uwekezaji mkoani Arusha, uliofanyika eneo la Olasiti.
“Watuhumiwa hawa siku si nyingi Kamanda wa Polisi wa Arusha, ataweka majina hadharani, watu wawajue na si wageni, ila kwa sasa kinachochunguzwa ni kutaka kufahamu waliowatuma kuingiza mabomu hayo na kwa lengo gani."
Mulongo alisema kwa sasa Polisi iko katika hatua za mwisho za mahojiano na watuhumiwa hao, ambapo mbali na kutaka kufahamu waliowatuma na malengo yao, pia wanatarajia kupata taarifa za waliorusha mabomu hayo.
Malengo mengine kwa mujibu wa Mulongo ni kuwafahamu watu wote waliopewa zabuni ya kuingiza mabomu hayo, ili hatua za kisheria zifuate.
Mulongo aliomba wananchi waendelee kutulia wakisubiri matokeo ya Serikali na hata wakitajwa wahusika waiachie Polisi ifanye kazi yake. Mabomu hayo yalirushwa Mei 5 kanisani Olasiti na Juni 15 uwanja wa Soweto, wakati wa hitimisho la kampeni za udiwani za Chadema mkoani hapa.

Tuesday, September 17, 2013

Polisi wawili wakamatwa na risasi 3,000




Mara. Polisi wawili wa Musoma, Mkoa wa Mara na Kibaha, Pwani wanashikiliwa kwa tuhuma za kukutwa wakisafirisha risasi 3,000 kutoka Musoma kwenda Dar es Salaam.
Wanaoshikiliwa kwa tuhuma hizo ni aliyekuwa mtunza chumba cha silaha Kikosi cha FFU Musoma na mwenzake mwenye cheo cha Koplo Wilaya ya Kibaha, Pwani. Inadaiwa walikamatwa Juni 2, mwaka huu saa 11:00 alfajiri.
Watuhumiwa wanashikiliwa Kituo cha Polisi Musoma na wamefunguliwa jalada MUS/RB/2465/013 wizi wa risasi 1,056, wanasubiri taratibu zingine za polisi.

Monday, September 16, 2013

Baada ya kumwaga Damu zaidi ya miaka 20, Somalia yakubali kukaa mezani,kujadili tofauti zao.

Mkutano kuhusu Somalia Brussels

EU kwa ushirikiano na serikali ya Somalia, Iimeandaa kongamano la kimataifa Brussels kutathmini hali maendeleo nchini Somalia dakika 45 zilizopita

http://www.bbc.co.uk/swahili/
Somalia imeshuhudia maendeleo si haba tangu Al Shabaab kufurushwa mjini Mogadishu.
Muungano wa Ulaya kwa ushirikiano na serikali ya Somalia, hii leo umeandaa kongamano la kimataifa mjini Brussels kutathmini hali inavyoendelea nchini Somalia
Wanadiplomasia wanasema wanatarajia kuwa wahisani wataahidi kuchangisha mamilioni ya dola kama msaada kwa Somalia kwenye mkutano huo.

Ufaransa: Syria lazima ishinikizwe zaidi kwani hali bado ni tete...!!!

Rais wa Ufaransa Francois Hollande ametaja makubaliano kati ya Marekani na Urusi kuhusu silaha za kemikali za Syria kama hatua muhimu katika suluhu kubwa zaidi la mgogoro wa kisiasa unaokumba taifa hilo.Lakini kwenye hotuba yake bwana Hollande aliongeza kusema kuwa "lazima wazo la kuchukulia Syria hatua za kijeshi lisalie , la sivyo hapatakuwa na shinikizo.’’

Sunday, September 15, 2013

AIBU :Dk. Mwakyembe aibua wizi mpya bandarini



WAZIRI wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, ameutaka uongozi wa Mamlaka ya Bandari ya Dar es Salaam kuvunja mara moja mkataba na Kampuni ya Ulinzi ambayo ilipewa zabuni ya kulinda bandarini hapo, baada ya kubainika kwamba baadhi ya walinzi wa Kampuni hiyo wanajihusisha na wizi wa mafuta katika boya la kupakulia mafuta lililoko baharini.

Kauli hiyo aliitoa jijini Dar es Salaam jana, katika mkutano wake na wafanyakazi wa Bandari, ambapo alisema wamegundua mtindo mpya wa kuiba mafuta unaofanywa na raia mmoja wa kigeni ambaye anashirikiana na walinzi wa Kampuni iliyoingia mkataba na Bandari ya Dar es Salaam.

Kauli ya Kanisa: Zanzibar haitaki Muungano,Lasononeka kuumizwa kwa matakwa ya kisiasa.


KANISA Katoliki Jimbo la Zanzibar, limesema matukio ya kigaidi yanayotekelezwa dhidi ya mapadri wa kanisa hilo, yana mkono wa kisiasa wenye lengo la kushinikiza visiwa hivyo kujiondoa katika Serikali ya Muungano.

Limesema upo ushahidi usiotiliwa shaka unaoonyesha kuwa, Wazanzibari wengi wanataka Muungano utoweke na visiwa hivyo viwe na Serikali yake kamili.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Jimbo la Zanzibar, Padri Arbogast Mushi, katika mahojiano yake na MTANZANIA Jumapili, yaliyofanyika katika viunga vya Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako Padri Anselmo Mwang’amba, amelazwa akipatiwa matibabu baada ya kumwagiwa tindikali juzi na watu wasiojulikana.

Saturday, September 14, 2013

KUNYONGWA HADI KUFA.:WALIOMBAKA MWANAFUNZI NDANI YA BASI WAHUKUMIWA KIFO ..!!!


Wanaume wanne jana wamehukumiwa kifo kwa kuhusika na shambulio la ubakaji na mauaji ya msichana kwenye basi mjini Delhi.

Jaji Yogesh Khanna, ambaye aliwatia hatiani wanaume hao kwa shambulio la ubakaji na 'kusababisha' mauaji mapema wiki hii, alikataa ombi la mwanasheria wao la kuwapunguzia adhabu wateja wake hao.


BONGO NOOMA! Mbinu mpya za kusafirisha dawa za kulevya zabainika...



KWA UFUPI
Imebainika kuwa miongoni mwa mbinu mpya wanazotumia ni kusafirisha dawa hizo kwa kutumia ndege za mizigo ambapo huweza kuweka dawa za kulevya kwenye mdoli, jarida, makopo ya maziwa ya watoto, vinyago vya kimakonde na kuutuma kama kifurushi kwenda sehemu nyingine.

“Wale wasafirishaji wa ndani ya nchi wanatumia njia kama hizo za kumeza, lakini wale manguli wanatumia meli za kukodi na ndege binafsi. Wanaweza kusafirisha hata kilo 800 kwa wakati mmoja,” alisema Nzowa.Wakati vyombo vya sheria vikiendelea kupambana na biashara ya dawa za kulevya nchini, wasafirishaji hao kila siku wanaendelea kuwa wabunifu na kubuni mbinu mpya na za kutisha za kusafirisha dawa hizo kutoka eneo moja hadi lingine.

KAULI YA UWOYA KWA SHIGOGO KWA KUMCHAFUA,DHIDI YA WIZI WA SIMU YA iPHONE 5



Ukurasa wa mbele wa gazeti la Risasi la leo Jumamosi (Sept 14) umetawaliwa na habari inayomhusu msanii wa Bongo Movie Irene Uwoya yenye kichwa cha habari “UWOYA MBARONI KWA WIZI WA SIMU!!

Hiki ni kipande cha habari hiyo kama ilivyoandikwa na gazeti hilo linalomilikiwa na Global Publishers:

Marekani yadai kugundua chanjo inayoangamiza VVU...!!!


KWA UFUPI
Katika majaribio ya chanjo hiyo, wanasayansi hao wameelezea kuwa imeonyesha mafanikio kwa kuangamiza kabisa virusi wanaofanana na VVU kwa nyani.

Washington. Wanasayansi nchini Marekani wamegundua chanjo ambayo wanaamini itaweza kuangamiza Virusi Vya Ukimwi (VVU) kwa binadamu.

Mbilimbi hutumika kufanyia mazoezi ya kubeba dawa za kulevya Jijini D’Salaam....!!!


Kulingana na utafiti uliofanywa na chanzo chetu, hii katika vijiwe, baadhi ya vijana wamebuni utamaduni wa kufanya mazoezi ya kubeba dawa za kulevya tumboni kwa kumeza mbilimbi bila kutafuna, ili iwapo itatokea nafasi ya aina hiyo muda wowote, wawe tayari kuingia kazini. Uchunguzi uliofanywa maeneo ya Kinondoni, Magomeni, Vingunguti, Manzese, Msasani, na Temeke, umegundua zao la mbilimbi limekuwa likitumika kama kifaa cha kupima uwezo wa mbebaji wa dawa za kulevya.

Thursday, September 12, 2013

Serikali yatangaza ajira mpya kwa walimu...!!!


SERIKALI imetangaza mpango mpya wa ajira za walimu 28,638 wa shule za msingi na sekondari, katika mikoa inayokabiliwa na changamoto ya uhaba wa walimu.

Mpango huo ulitangazwa juzi na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, wakati akizungumza katika mahafali ya nne ya Chuo Kikuu cha Elimu Mkwawa (MUCE) mkoani Iringa.

Wednesday, September 11, 2013

HUU NI UNYAMA: ANGALIA MAUAJI YALIYOFANYIKA SYRIA DHIDI YA RAIA HUSUSANI WATOTO...!!!


  1. In the Syria crisis, diplomacy currently holds center stage. US President Barack Obama yesterday said there were

     "Encouraging signs" 
    (New York) – Available evidence strongly suggests that Syrian government forces were responsible for chemical weapons attacks on two Damascus suburbs on August 21, 2013. These attacks, which killed hundreds of civilians including many children, appeared to use a weapons-grade nerve agent, most likely Sarin.

ONYO:SADC YAMUONYA KAGAME KUHUSU MPANGO WAKE WA KUIVAMIA TANZANIA KWA KUOMBA MSAADA WA KIJESHI


MZOZO wa kidiplomasia alioibua Rais wa Rwanda, Paul Kagame kwa Rais Jakaya Kikwete, sasa unaonekana kuchukua mwelekeo mpya, baada ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), kumuonya kiongozi huyo kuacha mara moja fikra zozote mbaya dhidi ya Tanzania, MTANZANIA Jumatano limedokezwa. 

Habari za uhakika na za kuaminika kutoka miongoni mwa viongozi wa juu wa SADC na maofisa wa Serikali, waliokuwa katika ujumbe wa Rais Jakaya Kikwete aliyekuwa akihudhuria Mkutano wa viongozi wa Maziwa Makuu huko Uganda hivi karibuni, zinaeleza kuwa tayari Jumuiya hiyo imekwisha mpatia ujumbe huo mmoja wa mawaziri aliyekuwa ameandamana na Kagame muda mfupi baada ya kikao chake na Kikwete.

Monday, September 9, 2013

STARTING AN ACTIVITY AND FORMALIZING A BUSINESS....!!!!


A LOT of discussion is often put up concerning how far informal sector operators pay tax, and it must take up some effort on the part of business educators to draw the line between what is civic to do . In a meantime, we need to ask what is necessary in terms of business activity.

The question that comes up is the link between civic duty and paying tax, and how this comes up when one starts an activity. For in the final analysis most small businesses start up simply as activities that are expected to generate incomes but not assured to succeed.

POST-MDGS ERA: AFRICA NOW NEEDS TO EVOLVE ITS OWN DEVELOPMENT AGENDA




COME September this year, and the United Nations’ member states will debate what should replace the Millennium Development Goals (MDGs) programme when it expires in 2015. The MDGs, instituted in the year 2000 by 189 UN member states, are the highest profile articulation of the internationally-agreed upon development goals. 

The UN development agenda set out to address extreme poverty, hunger, health, gender equality, education, environmental sustainability, and global partnership. According to the recently released UN MDG Report-2013 titled ‘Assessing Progress in Africa Towards the Millennium Development Goals, 2013,’ Africa is off-track in five of the goals. 

The continent has reportedly failed to meet almost 63 per cent of the goals in the period of 13 years. While the MDGs have demonstrated that, with resolve, the world can jointly rally around a common cause and achieve results, it is no secret that the former MDG dispensation was largely driven on an aid framework! If African states play their proper roles, there would be no need to subscribe to externally-generated development goals. 

Africans should, therefore, actively seek to evolve their own agenda that can transform the continent's vast potential — which is locked up in its people and natural resources — into sustainable progress.


Bilionea wa Afrika awekeza sekta ya madini Kenya....!!!!

KWA UFUPI

  • Waziri wa madini wa Kenya, Najib Balala alipongeza hatua hiyo ya Dangote na kufurahia ushirikiano wake na tume iliyoundwa na Serikali ya Kenya ya kuchunguza utaratibu wa utoaji leseni za kuwekeza katika sekta ya madini nchini Kenya. Balala  alitumia pia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji wengine katika sekta hiyo ya Madini,ili kusaidia kukuza uchumi wa nchi.

Serikali ya Kenya imewaalika wawekezaji wengine kujitokeza katika sekta ya Madini ili  kukuza uchumi.

Sunday, September 8, 2013

Unaweza kuboresha uwezo wako wa kukumbuka?

WA UFUPI

  • Aliweza kuzikariri sauti zetu wafanyakazi wote. Pia aliweza kuzikariri namba zetu wote na namba za ofisi na watu mbalimbali wa nje ambao tulikuwa tunamwomba atuunganishe tuongee nao.

Je, huwa unashindwa kukumbuka majina ya watu, namba za simu, tarehe za kuzaliwa watoto wako au nduguzo? Je, wakati mwingine unasahau mahali ulipoweka funguo. Kitabu chako cha benki au hata kitambulisho chako? Je, inatokea unasahau kama ulikuwa unapaswa kufanya jambo fulani wakati fulani?
Namkumbuka rafiki yangu tuliyekuwa tukifanya kazi pamoja aliyekuwa msahaulifu sana. Aliweza kuondoka kazini akaenda hadi nyumbani, kisha akakumbuka kuwa ufunguo wa chumba chake ameusahau ofisini. Siku nyingine, asubuhi alipanda basi akaenda hadi kazini na alipofika ndipo alipogundua kuwa ilikuwa siku ya Jumapili. Kila mara alipokwenda benki kwenye ATM alinipigia simu nimkumbushe namba yake ya siri ili aweze kuchukua fedha.

Maelfu hatarini kukosa mtihani kidato cha nne 2013


KWA UFUPI
Tayari Necta imetuma barua kwa watahiniwa hao kuwaeleza kuwa hawatafanya mtihani mwaka huu.
Dar es Salaam. Watahiniwa 3,000 wa kujitegemea wako hatarini kutofanya Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka huu kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) kutokuwa na taarifa zao za kulipia karo za mtihani huo pamoja na zile za usajili.Tayari Necta imetuma barua kwa watahiniwa hao kuwaeleza kuwa hawatafanya mtihani mwaka huu.
Licha ya maelezo hayo ya Necta, taarifa zinaonyesha kuwa watahiniwa hao walishalipa ada za mtihani huo kupitia njia mbalimbali za kielektroniki zilizoainishwa na baraza hilo, ikiwamo benki na kampuni za simu za mkononi.Watahiniwa walipaswa kulipa Sh35,000 ikiwa ni ada za mtihani huo kupitia wakala mbalimbali walioteuliwa na Necta.

Thursday, September 5, 2013

UNAJUA?? ...Machungwa, Zabibu Hupunguza Uwezekano wa Kupata Kiharusi



Utafiti uliofanyika nchini Marekani umesema ya kwamba kula machungwa na zabibu kunaweza kupunguza uwezekano wa kupata kiharusi (Stroke).
Utafiti huo uliangalia faida za matunda chachu (Citrus Fruit) pekee kwa mara ya kwanza tofauti na tafiti nyingi ambazo tumezizoea zinazoangalia umuhimu wa matunda na mboga za majani kwa afya kiujumla.

Matunda ni tiba kwako sio Anasa,... Magonjwa na Tiba kupitia Matunda!!




  • Hizi ni baadhi ya faida za kula matunda na zenye kuonyesha umuhimu na kuwavutia wengi kuyatumia kila siku.

Kwa jumla imezungumzwa au kuandikwa mara nyingi kuhusu umuhimu wa kula matunda ikiwezekana kabla ya kila mlo, lakini hiyo hainifanyi nishindwe kukumbusha kuhusu hilo.

Wednesday, September 4, 2013

MFANYA BIASHARA ANUNUWA NDEGE YA BOING 747 JUMBO NA KUIGEUZA KUWA NYUMA YA KULALA WAGENI


Ndani ya ndege hii "nyumba ya kulala wageni" kuna vyumba 27, unapata utandawazi, vyumba vina luninga, imesha aanza kuchukwa wageni wa kulala na ipo karibu na uwanja wa ndege wa  Arlanda airport karibu na mji wa Stockholm, Sweden




Nyumba hiyo ya wageni ambayo sasa iko tayari kwa biashara imewekwa karibu na uwanja wa ndege wa  Arlanda airport karibu na mji wa Stockholm, Sweden

Mmiliki wa ndege hiyo Oscar Divs alinunuwa ndege hiyo iliyoundwa 1976 Boeing 747-200 na kuibadilisha kuwa nyumba ya wageni 


Tuesday, September 3, 2013

AFRICA MUST RETHINK ITS GOVERNANCE SYSTEMS....!!!



SIX million Zimbabweans who are registered to vote were set to exercise their democratic right to choose their leaders across the country. It is commendable that President Robert Mugabe, Prime Minister Morgan Tsvangirai and Professor Welshman Ncube, the main presidential candidates, have all held their rallies in peace.

Teknolojia yenye manufaa kwa wakulima nchini,yagundulika..!!!


  • Mtafiti maarufu ndani na nje ya nchi katika masuala ya utafiti na magonjwa ya kilimo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo ya Mikocheni, Dk Joseph Nduguru, anasema kuwa teknolojia ya Uhandisi Jeni ina lengo la kuongeza mavuno kwa mkulima
  • Katika kitabu chake kiitwacho Starved for Science, How Biotechnology is being kept out of Africa, mwandishi Robert Paarlberg anaeleza sababu za wakulima wengi barani Afrika kuwa maskini kwa kuwa tu wameipuuzia teknolojia ya Uhandisi Jeni au kwa Kiingereza Genetically Modified Organism (GMO)

Wanafunzi Wauza vyuma chakavu kujisomesha


  • Kwa sababu ya wazazi wengi kutokuwa na mwamko wa elimu, hivyo kushindwa kuwahudumia watoto wao kielimu, wanafunzi wameamua kutafuta njia ya kupata mahitaji ya kielimu kwa kuuza vyuma chakavu wanavyobadilishana na kalamu na madaftari.

Uzoefu unaonyesha Mkoa wa Shinyanga, ni miongoni mwa mikoa iliyo nyuma kimaendeleo nchini.Hata katika sekta ya elimu, mkoa huo una historia isiyovutia. Kwa mfano, mara tatu mfululizo kuanzia mwaka 2009 hadi 2011, mkoa huo ulishika mkia katika matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi.

HAWA NDIO MATAJIRI 10 WANAOITIKISA ARDHI YA TANZANIA KWA PESA...!!


Said Salim Awadh Bakhresa.

KATI ya miaka ya 1960 hadi 1980, mtu kuwa tajiri alionekana ni hatari kwa taifa, tena mali zake alizimiliki kwa kificho, vinginevyo angeitwa mhujumu uchumi. Lakini kwa sasa mambo yamebadilika, taratibu sera za kibepari zinatawala, ujamaa unapewa kisogo.

Mtu kama ni mbunifu, ana nidhamu ya kutofuja pesa na anafanya kazi sana kwa nini asiwe tajiri? Utandawazi unasaidia ndiyo maana leo tunaweza kuwatambua mabilionea wakubwa ambao wanastahili pongezi kwa hatua walizopiga. Tusisahau kuwa wanaibeba nchi kwa ulipaji kodi.

1. SAID BAKHRESA

Jina lake kamili ni Said Salim Awadh Bakhresa. Jarida la Forbes mwaka jana, lilimuorodhesha miongoni mwa matajiri 40 Afrika kwamba anamiliki utajiri wenye thamani ya dola milioni 620 (karibu shilingi trilioni moja). Hata hivyo, inadaiwa kuwa tabia ya usiri wa Bakhresa inafanya mali zake zisijulikane sana, ila ni tajiri zaidi ya kiwango hicho.


Sunday, September 1, 2013

Tumejiandaa vipi na ‘uvamizi wa Wachina’?

KWA UFUPI
  • Kuna jeshi la Wachina linakuja, wako wengi. Kwenye moja ya picha za magazetini alipata kuonyesha Rais wetu akiwa amezungukwa na Wachina pale Ikulu.

Nitaanza kwa kukumbushia alichowahi kutamka Askofu Desmond Tutu. Aliyasema haya;“ Kuna tofauti ya kimsingi kati ya kuwa huru na kuwa katika hali ya kukandamizwa. Kuwa huru ni pamoja na kupata huduma za msingi za kijamii; kuwa na ajira, maji ya bomba, umeme, makazi bora na huduma za msingi za afya. Kuna maana gani basi ya kuwa huru wakati ubora wa maisha ya watu haujaimarishwa? Kama sivyo, hata kura nazo hazina maana yoyote!” – Desmond Tutu ( William Gumede; Thabo Mbeki And The Battle For The Soul Of The ANC, Uk. 67)

Tanzania Commission for Universities Call for Second Round Application!!

                          Tanzania Commission for Universities
                 Call for Second Round Through Central 
Admission System for Applicants who Have Not Been Selected During the First Round of Application due to Various Reasons.
1.Overview

TCU informs all applicants (Form six and applicants with foreign certificates) whose names have been published on TCU website that, they have not been selected in all of their choices due to various reasons including:
i) Being eligible but left due to Competition;
ii)Failure to submit their programme choices;
iii) Choosing programmes that they do not qualify.
**********PLEASE CLICK THE LINK  LEFT**********

Nafasi za Kazi.....50 Posts!!!

QUALITY IMPROVEMENT ADVISORS  -  3  POSITIONS
Qualifications: First degree in clinical training who have the skills in continuous quality improvement training and mentorship
Apply:  The Chief of Party
URC-Mwanza
Box  1403 Mwanza or
hrmwanza@urc-chs.com
Details:The Guardian, Aug 21, 2013  
Deadline:  September   15, 2013

ENGINEER  II,  MOVABLE  ASSETS
Qualifications: Mechanical
Engineering qualifications at degree level, registered with
Engineer’s Registration Board
Apply:  The Managing Director Reli Assets Holding Company Ltd
Box  76959 , Dar es Salaam
Details: Mwananchi, Aug 22 , 2013  
Deadline:  September   6, 2013

Benki Ulaya yaipiga jeki NMB kusaidia wajasiriamali

KWA UFUPI
  • Alisema kuwa NMB itakuwa ikitoa Sh32 milioni kwa mwezi kwa ajili ya kusaidia wafanyabiashara  wadogo na wa kati vikiwamo viwanda vidogo vya usindikaji mazao, huduma na wazalishaji mali na  mara nyingi mikopo hiyo huwa chini ya mwaka mmoja.

SINGLE CUSTOMS TERRITORY WITHIN EAC TAKING SHAPE

KAMPALA – Members of the business community engaged in cross-border trade within the East African Community countries of Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi and Tanzania are well-positioned to start enjoying smooth trade flows in earnest when the concept of a Single Customs Territory (SCT) becomes operational. Under that arrangement, the EAC member states will adopt a destination model of clearance of imports whereby the assessment and collection of tax revenues on such consignments will be done at the first point of entry.