Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, September 16, 2013

Baada ya kumwaga Damu zaidi ya miaka 20, Somalia yakubali kukaa mezani,kujadili tofauti zao.

Mkutano kuhusu Somalia Brussels

EU kwa ushirikiano na serikali ya Somalia, Iimeandaa kongamano la kimataifa Brussels kutathmini hali maendeleo nchini Somalia dakika 45 zilizopita

http://www.bbc.co.uk/swahili/
Somalia imeshuhudia maendeleo si haba tangu Al Shabaab kufurushwa mjini Mogadishu.
Muungano wa Ulaya kwa ushirikiano na serikali ya Somalia, hii leo umeandaa kongamano la kimataifa mjini Brussels kutathmini hali inavyoendelea nchini Somalia
Wanadiplomasia wanasema wanatarajia kuwa wahisani wataahidi kuchangisha mamilioni ya dola kama msaada kwa Somalia kwenye mkutano huo.


Mkutano huo unawaleta pamoja maafisa wa serikali , mashirika ya misaada na taasisi za kifedha.
Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud, aliambia BBC kuwa mkataba mpya unaopendekezwa na ambao unaipa nchi hiyo usemi mkubwa kuhusu mahitaji yake ya maendeleo, utaifaidi nchi ya Somalia pakubwa sana.
Duru zinasema kuwa matatizo chungu nzima yangali yanaikumba Somalia ikiwemo serikali kudhibiti sehemu ndogo tu ya nchi na ripoti za utumizi mbaya wa pesa.

 BBC

No comments:

Post a Comment