Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, September 3, 2014

FURSA: NHC yagawa mashine za kufyatulia matofali

Tanga. Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limeanza kugawa mashine za kisasa za kufyatulia matofali katika halmashauri za mkoani Tanga, huku likiwataka vijana kuzitumia kama sehemu ya ajira yao.
Meneja wa NHC mkoani Tanga, Issaya Mshamba aliyasema hayo juzi mjini Muheza alipokuwa akikakabidhi mashine hizo kwa mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, Ibrahim Matobu.
“Shirika la Nyumba limeamua kuwakumbuka vijana kwa kuwaletea mashine hizi ili waweze kujiajiri kupitia vikundi vitakavyosimamiwa na halmashauri zao, kwa hiyo ni vyema wazitumie kwa manufaa yao na Taifa kwa jumla,” alisema Mshamba.
Alisema NHC imetoa mashine 40 zitakazogawiwa katika halmashauri 10 na inatarajia kuwa vijana ndiyo watakuwa wa kwanza kunufaika.
Akizungumza baada ya kupokea mashine hizo, Matovu alisema kila kikundi kitakachokabidhiwa mashine, atakitafutia zabuni ya kusambaza matofali.
“Hatuwezi kuwaacha hivi hivi, lazima tuwatafutie zabuni katika taasisi mbalimbali,” alisema.

Source: m'nchi

No comments:

Post a Comment